
Utafiti
uliofanywa na profesa Charles Gerba wa chuo kikuu cha Arizona nchini
Marekani umebaini kwamba wengi wetu hususan sie kina mama hatusafishi
mikoba yetu tunayotumia kufanyia manunuzi sokoni. Kuna hii mifuko
maarufu kwa jina la mifuko ya Rambo au wakati mwingine tunayo mikoba
maalum ya Canvas ambayo tunaitumia kufanyia manunuzi. Mikoba hii huwa
tunaitumia na kisha kuihifadhi kwa matumizi wakati mwingine.
Profesa
Gerba ambaye ni mtaalamu wa masuala ya udongo, maji na mazingira,
alichunguza na kupima zaidi ya mikoba 100 kwenye miji ya California na
Arizona, na katika utafiti huo aligundua kwamba ni asilimia 3 tu ndio
wanaosafisha mikoba yao. Katika utafiti huo aligundua mikoba mingi ikiwa
na vijidudu hatari vya Coliform asilimia 50 na E. Coli asilimia 8
“Inashangaza kidogo kuona mtu anatumia mikoba hiyo kubebea nyama, mayai, mboga mboga ambazo hata hazijaoshwa vyema na makorokoro mengine ambapo yamesheheni vijidudu vya maradhi lakini haifanyii usafi mikoba hiyo, bali huiweka kwa matumizi wakati mwingine.” Alisema Mtaalamu huyo wa masuala ya udongo, maji na mazingira,
Profesa Gerba alishauri watu wawe wanaosha mifuko yao kwa sabuni na maji ya moto baada ya matumizi.
“Inashangaza kidogo kuona mtu anatumia mikoba hiyo kubebea nyama, mayai, mboga mboga ambazo hata hazijaoshwa vyema na makorokoro mengine ambapo yamesheheni vijidudu vya maradhi lakini haifanyii usafi mikoba hiyo, bali huiweka kwa matumizi wakati mwingine.” Alisema Mtaalamu huyo wa masuala ya udongo, maji na mazingira,
Profesa Gerba alishauri watu wawe wanaosha mifuko yao kwa sabuni na maji ya moto baada ya matumizi.
0 comments:
Post a Comment