Mwanamke akipata chanjo ya homa ya ini, ugonjwa ambao unaua na kusumbua wengi duniani ikiwamo Tanzania. Picha ya Mtandao
Kwa ufupi Wataalamu wanaeleza kuwa Hepatitis B au homa ya
ini ni ugonjwa unaoambukizwa kwa urahisi, wenye madhara makubwa na
wenye uwezo wa kuambukiza kwa wepesi kuliko Ukimwi.
Ugonjwa wa selimundu unasumbua wengi, umetengua ndoa za wengine, kwa sababu ya kutojua.
Kwa wengine, chanjo hiyo ikiwamo ya homa ya ini
imeonekana kama usumbufu na udhia mtupu. Hata hivyo, wapo wengine ambao
hawaufahamu ugonjwa huu.
Kwa wanaoujua, wanahofia kuwa ugonjwa huu una madhara makubwa pengine kuliko saratani na Ukimwi.
Homa hiyo au Hepatitis B inapewa uzito mdogo licha ya kuwa ni ya hatari kubwa.
Wataalamu wanaeleza kuwa Hepatitis B au homa ya
ini ni ugonjwa unaoambukizwa kwa urahisi, wenye madhara makubwa na wenye
uwezo wa kuambukiza kwa wepesi kuliko Ukimwi.
Kitaalamu, ugonjwa huu, husababishwa na virusi vya
Hepatitis B (HBV) ambavyo huathiri mfumo wa utoaji wa sumu mwilini.
Inaelezwa kuwa robo tatu ya watu ulimwenguni wameathiriwa kwa muda na
homa ya ini na wengine milioni 350 wameathirika moja kwa moja.
Takwimu zinaonyesha kuwa homa ya ini huua watu
600,000 kila mwaka katika sehemu mbalimbali, idadi ya watu inayolingana
na wale wanaokufa kutokana na malaria.
Maradhi haya ya ini yanaelezwa kuwa yanaweza kusababishwa na kunywa kileo kupita kiasi au sumu inapoingia mwilini.
Hata hivyo, mara nyingi ugonjwa huu husababishwa na virusi.
Wanasayansi kwa upande mwingine wamegundua virusi
vitano vinavyosababisha ugonjwa huu na wanasema kwamba huenda kuna
vingine vitatu.
Matokeo yake, sheria zimewekwa katika nchi
mbalimbali ambazo zinamtaka kila raia mgeni anayetaka kuingia katika
nchi husika, kupata chanjo ya ugonjwa huu ili kuepusha maambukizi.
chanzo Mwananchi |
Thursday, 14 August 2014
- Blogger Comments
- Facebook Comments
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment