-

-

-

-

-

Habari Mpya

Wednesday, 6 August 2014

MARADHI YA NGOZI KWA NJIA YA NGONO

Baadhi ya maswali tuliyopokea, mengi yalihusu maradhi ya sunzua ambayo kitaalmu yanajulikana kama warts. 

 
Sunzua ni ugonjwa wa ngozi unaofahamika na wengi. Ugonjwa huu husababishwa na virusi ambavyo kitaalamu huitwa human papilloma virus.
Karibu asilimia 10 ya wanadamu wamewahi kupata athari za virusi vya ugonjwa huu, achilia mbali kuumwa sunzua.

afyatele
Kwa sababu hiyo ndiyo kusema kila mtu anapaswa kufahamu ugonjwa huu kwa undani ili unapojitokeza awahi hospitali ili kuudhibiti.
 
Virusi vinavyosababisha ugonjwa huu huambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya ngono.
 
Ugonjwa huu hutokea sehemu mbalimbali za mwili, lakini huwatokea wengi sehemu za siri.
 
Sunzua kama ugonjwa wa zinaa, huathiri sehemu za siri pamoja na njia ya haja kubwa.
 
Wagonjwa ambao wanaishi na Virusi vya Ukimwi wako kwenye mazingira hatarishi zaidi ya kupatasunzua.  
 
Virusi vinavyosababisha maradhi ya sunzua huambukizwa kwa njia ya ngono na ni mara chache huweza kusambaa kwa njia ya kugusana.
 
Virusi wa maradhi haya wanajulikana kama papilloma na hujitokeza kwenye eneo la ngozi ambapo virusi hivi vimepenya. Mara nyingi hujipachika kwenye mchubuko au mpasuko wa ngozi.
 
Maradhi haya huweza kujitokeza kwenye ngozi kati ya miezi miwili hadi tisa baada ya kupenya kwenye ngozi.
 
Maradhi haya husababisha ngozi kutokuwa na muonekano wake wa kawaida.
 
kwa hisani ya ulimwengu wa vijana blog
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: MARADHI YA NGOZI KWA NJIA YA NGONO Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top